JIFUNZE MAAGANO MUNGU ALIYOYAFANYA NA MWANADAMU KATIKA AGANO LA KALE

 

Je unayafahamu maagano ambayo Mungu alifanya na watu wake na maana yake? Kama bado, basi waweza kujifunza hapa kwenye makala ya leo. Pia waweza kushare na mwenzako ili naye aweze kujifunza zaidi juu ya maagano haya ambayo Mungu alifanya na wanadamu ili kuendeleza, kuratibisha, kusimamia, na kueneza ufalme wake toka Mbinguni hadi duniani alipo mwanadamu aliyemuumba kwa mfano wake. Pale tunaposali sala ya Baba yetu wa mbinguni kwa kusema ‘Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe duniani kama huko Mbinguni’ huu ndio ufalme wa Mungu tunao uzungumzia. Mungu kupitia maagano yake na mwanadamu alikua akisimamia na kueneza ufalme wake hapa duniani. Katika maagano haya tumajifunza ushirikiano wa Mungu na mwanadamu katika usimamizi na utawala wa ufalme wake.


Ni ngumu sana kuwakuta wakristo katika ulimwengu wa sasa wakizungunza kuhusu maagano. Lakini ukweli ni kwamba, sisi kama wakristo katika kanisa la Kristo yatupasa kukumbuka na kuyajadili maagano haya ambayo Mungu alifanya na wanadamu. Maagano ni mojawapo ya mada muhimu sana katika Biblia kwani ndio msingi wa kuelewa zaidi hadithi nzima ya ukombozi katika Biblia. Ukombozi wetu kwa Kristo umejengwa katika msingi wa maagano haya.


Tukitazama kuanzia kitabu cha Mwanzo katika Biblia na kuendelea, tunaona Mungu akiingia katika uhusiano mmoja baada ya mwingine (yaani, maagano) na wanadamu mbalimbali ili kuokoa ulimwengu wake na kuendeleza ufalme wake duniani.


Maagano ya Mungu katika Biblia


Kuna maagano mengi katika Biblia, lakini katika makala hii tutaangazi maagano matano muhimu kwetu ambayo yanatusaidia katika kuelewa hadithi ya Biblia na mpango wa Mungu katika kuleta ukombozi kwa mwanadamu aliyepotea na kusimamia na kueneza ufalme wake duniani. Maagano hayo ni: Agano na Adamu, Agano la Nuhu, Agano la Ibrahimu, Agano la Musa, Agano la Daudi, na Agano Jipya. Lakini makala hii itaangalia zaidi maagano yaliyopo katika agano la kale, kisha hapo baadae tutakua na makala ya pili ambayo itaangazia kwa kina agano jipya.


Agano na Adamu – Agano la msingi


Agano lakwanza katika Biblia ni Agano ambalo Mungu alifanya na Adamu (Mwanzo 1-3, Hosea 6:7), Hili lilikuwa ni agano la msingi kwa mwanadamu na msingi wa maagano mengine yote yaliyofuata baadaye. Agano hili lilitoa malengo ya Ufalme wa Mungu na wajibu na majukumu ya mwanadamu katika ufalme wa Mungu hapa duniani kabla na baada ya mwanadamu kutenda dhambi na kwenda kinyume na Mungu. Katika Agano na Adamu, mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu ili kuratibisha shughuli na kueneza ufalme wa Mungu ulimwenguni kote (Mwanzo 1:27-28, 5:1-2).


Wanatheolojia wanaliita agano hili ‘Agano la Mungu na Adamu’ kuwa ni agano la kazi kwa sababu linatokana na kanuni ya utii wa Adamu. Wapo wachache ambao husema kuwa Mungu hakufanya Agano na Adamu na hii ni kutokana na kuwa Mungu hapo mwanzo hakutumia neno ‘Agano’ katika jambo lolote alilosema kuhusu Adamu. Lakini katika Hosea 6:7, tunaamini kuwa Mungu alifanya Agano na Adamu. Kutokuwepo kwa neno "agano", katika kumbukumbu za kibiblia hasa katika kitabu cha Mwanzo haimaanishi kwamba hakuna agano lililokuwepo. Hata baada ya Adamu na Hawa kufukuzwa kutika katika bustani ya Edeni, waliendelea kuwa chini ya agano hilo. Biblia inatuonyesha fika kuwa toka uzawa wa Adamu na kuendelea Mungu aliendelea kufanya maagano na watu wake.


JIFUNZE ZAIDI JUU YA AGANO HILI 'KWA KUBOFYA HAPA'


Agano na Nuhu – Agano na viumbe wote, Ahadi ya kutoharibiwa kwa ulimwengu  


Agano la pili katika Biblia Mungu alilifanya na Nuhu (Mwanzo 6:18;9:9-17), baada ya Gharika, Mungu alifanya agano lingine na Nuhu, Agano la utulivu (stability). Hili linajulikana kama agano la Nuhu. Ukisoma Mwanzo 9, hili ni agano ambalo Mungu anaweka na Nuhu baada ya gharika ambapo anafanya upya kwa kudhibitisha baraka za uumbaji, sura ya Mungu ndani ya mwanadamu na kazi ya kutawala nchi. Mungu anaingia katika uhusiano (Agano) na Nuhu na viumbe vyote hai akiahidi kwamba licha ya uovu wa wanadamu hatawaangamiza tena, kwamba hatoiangamiza tena dunia kwa maji (gharika) wala kuilaani nchi, na kama ishara ya agano alilofanya na Nuhu, Mungu “akaweka upinde wake mawinguni.


Pia Kama ilivyokuwa kwa agano lake na Adamu hapo awali, katika Agano hili Mungu alilifanya kwa upya Agano lake na Adamu kwa Nuhu. Nuhu na familia yake waliamriwa waijaze dunia. Kwa Agano hili Mungu aliahidi kutawala juu ya dunia kwa wanadamu na uzima wa milele kama malipo ya utii. 

 

Agano la Nuhu lina sifa tatu za msingi. Kwanza, ni agano lisilo na masharti, na hii ni kutokana na kwamba halikutegemea chochote ambacho Nuhu au uzao wake ungefanya ili kulitimiza agano. Pili, lilikua ni agano lililofanywa kwa Nuhu na uzao wake wote pamoja na “kila kiumbe hai” na dunia nzima kwa ujumla (Mwanzo 9:8-10). Tatu, Agano hili lilitiwa muhuri kwa ishara ya upinde wa mvua. Ahadi za agano hili zilitegemea uaminifu wa Mungu peke yake na si vinginevyo. Hili ni Agano kati ya Mungu na kila kiumbe duniani (Mwanzo 9:17).


Soma zaidi: Mwanzo sura ya 8:20-9:17


Agano na Ibrahamu – Ahadi na Kuzaliwa kwa Taifa la Israeli


Agano la tatu ni Agano kati ya na Abrahamu (Mwanzo 15,17). Katika Agano hili Mungu anamuahidi Ibrahimu nchi, uzao na baraka. Agano hili ni agano la kuchaguliwa kwa Israel kuwa taifa ambalo Mungu atalitumia katika kueneza na kuratibisha ufalme wake hapa duniani. Katika agano hili Mungu aliahidi kuwa angembariki Ibrahimu kwa njia tatu. Sehemu ya kwanza ya agano hili inajulikana kama nchi ya ahadi ya Kanaani (Mwanzo 12:1, Mwanzo 15:7), ambapo Ibrahimu anaitwa na Mungu kutoka katika nchi ya baba zake Uru na kwenda mahali panapojulikana kama Kanaani. Nchi ambayo baadaye ilijulikana kama Israeli. 


Ahadi ya pili ni kuwa Mungu angemfanya kuwa taifa kubwa (Mwanzo 12:2 - Hapa ndipo Mungu alipoahidi kwamba angefanya taifa kubwa kutoka kwake, na hapa ndipo Mungu alipobadilisha jina la Abramu kuwa Ibrahimu likimaanisha ‘baba wa mataifa mengi) na hivyo kulifanya jina lake kuwa kuu, na hatimaye baraka ya tatu ni kuwa kupitia yeye Mungu angebariki mataifa mengine (Mwanzo 12:3).


Kama sehemu ya agano hili na Ibrahimu, Mungu alimwambia Ibrahimu kuondoa govi lake na govi za wavulana wote wa Kiyahudi baada yake. Utaratibu huu unajulikana kama tohara/kutairi na ni ishara ya agano la Ibrahimu na Mungu. Kulielewa Agano hili ni muhimu sana katika kuelewa dhana za kitheolojia kama vile Nchi ya Ahadi, uchaguzi wa wana wa Israeli, watu wa Mungu, urithi na kadhalika. Kulielewa agano hili kunatoa muktadha wa kuelewa zaidi desturi kama vile tohara, migogoro na mataifa yaliyowazunguka na migawanyiko kati ya Wayahudi na mataifa mengine.

Soma zaidi: Mwanzo sura ya 12, 15, and 17

 

Agano na Musa – Mwanzo wa Sheria kwa watu wa Mungu/Taifa la Israeli  


Agano la Nne ni Agano kati ya Mungu na Musa pamoja na wana wa Israeli. Agano hili linatambulika kama Agano la Musa (lililoitwa baada ya Musa), ambalo pia linajulikana kama agano la Sinai (linaloitwa baada ya Mlima Sinai wa Biblia), ni agano ambalo Mungu aliliweka na wana wa Israeli kwenye Mlima Sinai baada ya kuwatoa utumwani Misri. Mungu aliwakomboa wana wa Israeli kutoka utumwani Misri na kuahidi kuwafanya kuwa mali yake mwenyewe yenye kuthaminiwa, taifa takatifu, lililotengwa kwa ajili yake, kwa kazi maalumu ya kueneza ufalme na utukufu wake ulimwenguni. Yeye (Yahwe) atakuwa Mungu wao na wao (Israeli) watakuwa watu wake.


Walipokuwa wakitembea kutoka Bahari ya Shamu hadi nyikani, Wana wa Israeli hawakujua ni nini walichotarajia, lakini walipofika chini ya Mlima Sinai, waligundua kwamba Mungu alikuwa amechagua mahali hapa ili kujidhihirisha kwao na kuingia katika agano nao.


Mungu alimchagua na kufanya agano na Musa ( Kutoka 19-24) pamoja na wana wa Israeli. Musa na watu wake walipofika Mlima Sinai baada ya kutoka Misri kuelekea Nchi ya Ahadi, Mungu alizungumza na Musa. Hapa ndipo Mungu alipofanya agano na Musa na watu wake ambalo lililifanya upya lile alilokuwa amefanya na Ibrahimu. Wakati huo huo, Mungu aliwapa Amri Kumi – kanuni na sheria ambazo walipaswa kuishi nazo kama taifa teule la Mungu. Sheria ambazo ziliwaunganisha wayahudi wote kuwa taifa moja la Israeli. Sheria ambayo ilikusudia kuwatawala na kuwafanyiza watu wa Israeli katika Nchi ya Ahadi. Sheria hii haikuwa njia ya wokovu bali iliwatenga na kuwatofautisha na watu wengine wa mataifa yaliyowazunguka, hii ilikuwa ni kuwafanya kuwa taifa pekee la makuhani wa Mungu (Kutoka 19:1-7) katika kuendeleza ufalme wa Mungu hapa duniani. Agano hili lilikuwa na masharti na lilifafanuwa baraka na laana ambazo wangepokea kulingana na utii au kutotii (Kumbukumbu la Torati 28-29).


Agano ambalo Mungu alifanya na Musa lilijengwa juu ya agano alilofanya na Ibrahimu, na kwa agano hili, Mungu aliwaongoza wana wa Israeli kuielekea nchi yao ya ahadi.


Soma Zaidi: Kutoka Sura ya 19-24


Agano na Daudi – Agano la kifalme  


Agano la tano na la Mwisho kwa Makala ya leo ni Agano kati ya Mungu na Mfalme Daudi (nyumba/uzao wa Daudi). Mungu alifanya agano na mfalme Daudi (Zaburi 89, 132). Agano lake na Mfalme Daudi ni agano ambalo liliwafanya Daudi na uzao wake kuwa warithi wa kifalme katika taifa la Israeli Daima (2 Sam. 7:12-13). Katika Agano hili kwa kifupi ni kwamba Mungu anamweka Daudi kuwa mfalme juu ya Israeli na kuahidi kufanya jina lake kuwa kuu. Anaahidi kumpa Daudi ufalme wa kifalme ambamo kupitia kwake ahadi zilizotolewa kwa Ibrahimu na Israeli zitatimizwa kupitia ukoo wake. Ni agano ambalo Mungu anaahidi mzao wa Daudi kutawala katika kiti cha enzi juu ya watu wa Mungu. Kupitia agano hili nchi ya Israeli iliendelea kupanua mipaka yake na kuwa taifa imara na lenye nguvu.


Agano hili linakuwa msingi wa tumaini la Masihi na linaleta maana ya hangaiko la Injili kuonyesha Yesu alikuwa Mfalme halali wa Wayahudi. Agano hili lilitimia pale Yesu Kristo, mzao wa uzao wa Daudi, alipozaliwa katika Bethlehemu. Injili ya Mathayo inaanza kwa kuonyesha Kristo alikuwa “Mwana wa Daudi” (Mt. 1:1), na hivyo alikuwa na haki ya kutawala watu wa Mungu. Petro alihubiri kwamba Yesu Kristo alikuwa utimilifu wa ahadi ya Mungu kwa Daudi (Matendo 2:29-36).


Soma zaidi: 2 Sam 7; Zab 72, 89, na 132


Kwanini Maagano haya?


Wote ambao Mungu alifanya nao agano walikua ni wawakilishi wa wanadamu wengine mbele za Mungu. Maagano haya yalifanyika ili Mungu aweze kueneza na kuratibisha ufalme wake toka mbinguni hadi duniani kupitia mwanadamu.


Agano la Mungu kati ya Adamu na Nuhu (Mungu na Adamu/Mungu na Nuhu) yanatambulika kama maagano na ulimwengu wote/mzima (universal covents – kwa lugha ya kiingereza), kwani maagano haya yalihusisha wanadamu wote duniani. Adamu na Nuhu waliwawakilisha wanadamu wote kuwa ni watu wa Mungu katika maagano haya. Na kama tunavyotambua, kila agano la mungu lililotangulia liliendelea kuwa msingi wa agano lililofuata. Maagano yote yaliyofuata yalijengwa juu ya maagano ya nyuma yake. Agano na Nuhu liliendelea kujengwa juu ya Agano na Adamu, nk.


Agano la Mungu kati yake na Abrahamu, Musa, na mfalme Daudi yanatambulika kama maagano ya kitaifa (national covenants – kwa lugha ya kiingereza). Katika maagano haya wahusika waliwawakilisha wana wa israel pamoja na wale walioingia katika taifa la israel kama wateule wa Mungu. Mungu alichagua taifa la Israel kuwa chombo chake cha kueneza na kuendesha ufalme wake hapa duniani. 


Kwanini ni muhimu kwa mkristo kuyafahamu maagano haya?


Kuyafahamu maagano haya ni Muhimu kwa Mkristo kwasababu yanatuwezesha sisi kuona ni kwa jinsi gani hadithi za Biblia zina umoja katika kudhihirisha ufalme wa Mungu na ahadi zake kwa mwanadamu, hasa katika ahadi ya ukombozi wa mwanadamu kutoka katika dhambi na mateso. Pia inatusaidi kuuona uaminifu wa Mungu toka kuwepo kwa misingi ya ulimwengu. Mungu ni MUNGU wa maagano, ni Mungu mwaminifu, na ni Mungu ambaye hadi sasa hutimiza maagano na ahadi zake kwetu sisi wanadamu.

 

Kama una swali au ushauri juu ya Makala hii usisite kuwasiliana nami, nipo tayari kukusaidia kuelewa zaidi na kujifunza juu ya ufalme wa Mungu. Pia kadri tunavyoendelea kujifunza tutachambua maagano haya kwa kina zaidi kwa kuliangazia moja baada ya lingine hapo baadae. Endelea kusoma blog hii kujifunza zaidi.


Kwasababu ya Kalvari mimi nimewekwa Huru,

Rumishael Ulomi

Copyright © www.kilicentric.com


Makala hii ipo kwa lugha ya KIINGEREZA HAPA

R

Rumishael Ulomi

Author, Coach & Minister

Rumishael Ulomi is a seasoned leader and minister dedicated to integrating Christian values into leadership and life. He empowers individuals to reach their God-given potential through discipleship, coaching, and mentorship.

KiliCentric

The official blogof Rumishael Ulomi aka RyChris, hailing all the way from Moshi Kilimanjaro. .

Search This Blog

Labels

Follow Us

Should Your Religion Be Based On Your Feelings? Here is the answer..

Should a person decide what to believe based on his or her feelings or something that does not change with moods and circumstances? Big question! Imagine Jesus of Nazareth nailed up on the cross, dying for our sins. Suppose He said, “This is not fun. I am not feeling anything good up here. Let me off this cross. I expected good feelings, not this! Pain is not where it is at for Me. My commitment to die to pay the penalty for man’s sin is far beyond what I am feeling right now.” How would you have counseled Jesus when the bad pain hit Him? Feelings based religion is shaky. Commitments based on good feelings are subject to change any day. This unbiblical approach would make all our commitments very tentative, unpredictable, shaky. This includes: marriage, family, job and friends. A marriage vow would only mean, “I’ll stay with you as long as my good feelings last. I expect only good times, no bad ones.” Jesus did not bail out when the going got tough. Some beliefs a Christian should also...

The second necessary step in designing a successful nonprofit strategy is knowing your beneficiaries

Last week I started a series of blog posts on building a strong and successful strategy for your nonprofit and I started with mentioning the first necessary step you will need to examine before kicking off with your strategy. If you haven’t read that post, I recommend that you visit the article HERE before continuing with this one. Having familiarity with the first article will help you understand this one even much better. This week we are looking at the second step to take when designing your nonprofit strategy, and that step in designing and building a strong and successful strategy for your nonprofit is clearly knowing, stating, and understanding who your beneficiaries are. Some organizations talk about beneficiaries, others refer to participants, others to clients, service users or partners. Here we will refer to beneficiaries as the people whom your nonprofit seeks to benefit. The reason why many nonprofit strategies fail is because too often nonprofits and funders ignore the con...

Being set free by the master who holds the keys to life

After Jesus died on the cross He went down to hell, crushed the devil, and took the keys of life. The devil held us prisoners to fear of death, but now we are given the chance to enjoy eternal life with God the father. The greatest gift the human race can ever earn. It’s all free of charge to be set free, for the master has promised to do this free of charge to all those who desire to be free. If you have not yet accepted Christ, then you are still in a prison cell and you need to be freed from this. The only way that can happen is if you humble yourself and come to the master who has the keys to set you free. If you are in the devils prison, you can’t save yourself, not matter how good you think you are in escaping. You will never be able to escape until you let the master who took the keys set you free. You will try million ways and times, but I assure you, you will never succeed on your own. Many of you may say ‘well I am free’, I can assure you that you are only free in the flesh; ...

Join the Sikio Sikivu Diary

Get weekly leadership insights, biblical management tools, and discipleship resources delivered straight to your inbox.

No spam, just wisdom. Unsubscribe anytime.