JIFUNZE ZAIDI JUU YA AGANO LA MUNGU NA ADAMU

 


Katika Makala iliyopita tulijifunza juu ya maagano ya Mungu aliyofanya na mwanadamu ili kusimamia, kuratibu, na kueneza ufalme wake duniani. Maagano haya yalikua ni yale yaliyofanyila katika Agalo la kale, kama haujafanikiwa kuisoma Makala hii tafadhali BOFYA HAPAKUISOMA.


Tulijifunza kuwa, Agano la kwanza ambalo Mungu alifanya na mwanadamu katika Biblia ni Agano alilolifanya na Adamu (Mwanzo 1-3, Hosea 6:7), Hili lilikuwa ni agano la msingi kwa mwanadamu na lilikuwa ni msingi wa maagano mengine yote yaliyofuata baadaye. Agano hili lilitoa malengo ya Ufalme wa Mungu na wajibu na majukumu ya mwanadamu katika ufalme wa Mungu hapa duniani kabla na baada ya mwanadamu kutenda dhambi na kwenda kinyume na Mungu. Katika Agano na Adamu, mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu ili kuratibisha shughuli na kueneza ufalme wa Mungu ulimwenguni kote (Mwanzo 1:27-28, 5:1-2). Mungu aliumba ulimwengu na wanadamu, akionyesha yeye ndiye mtawala mkuu wa wote na vyote alivyoviumba. Aliwaumba Adamu na Hawa wakiwa makuhani-wafalme, kama wale waliofanywa kwa mfano wake, wautawale ulimwengu kwa ajili ya Mungu. Walipaswa kupanua utawala wa Mungu juu ya dunia yote.


Wapo wachache ambao husema kuwa Mungu hakufanya Agano na Adamu na hii ni kutokana na kuwa Mungu hapo mwanzo hakutumia neno ‘Agano’ katika jambo lolote alilosema kuhusu Adamu. Lakini Tumshukuru Mungu kuwa kupitia Nabii Hosea katika Hosea 6:7, anatuelimisha juu ya hili na tunaamini kuwa Mungu alifanya Agano na Adamu. Kutokuwepo kwa neno "agano", katika kumbukumbu za kibiblia hasa katika kitabu cha Mwanzo haimaanishi kwamba hakuna agano lililokuwepo. Kupitia Hosea tunajifunza kwamba Agano la kwanza ambalo Mungu aliwahi kufanya na wanadamu lilikuwa ni Agano na mwanadamu wa kwanza, Adamu mwenyewe.


Wanatheolojia wanaliita agano hili ‘Agano la Mungu na Adamu’ kuwa ni agano la ‘kazi’ kwasababu linatokana na kanuni ya utii wa Adamu. Sehemu ya kwanza ya Agano la Adamu ilikuwa na Baraka nyingi muhimu zilizoambata na onyo kwa Adamu. Adamu na Hawa waliumbwa kwa mfano wa Mungu, na kupewa mamlaka juu ya uumbaji wa Mungu, lakini kuna mambo ambayo walipaswa kutekeleza.


Mungu aliwabariki Adamu na Hawa kwa kuwaweka katika bustani nzuri yenye malisho ya kila aina, katikati ya mito minne iliyojawa na maeneo yenye kupendeza na kuvutia kuanzia miti mizuri hadi mawe ya thamani. Zaidi ya yote Mungu aliwapa hadhi kubwa sana kwa kuwapa jukumu la kutawala uumbaji wake na kuijaza dunia kwa uzawa wao. Mungu anawapa zawadi ya uhusiano na uwezo wa kuzaa watoto na kuijaza dunia. Mungu alitoa mamlaka ya kuratibisha na kueneza ufalme wake duniani kwa Adamu na Hawa. Mungu alikuwa aeneze ufalme wake duniani kupita Adamu na Hawa.


Onyo ambalo Mungu alitoa kwa Adamu ni kuhakikisha kuwa hawali tunda la mti wa mema na mabaya, kwani siku ambayo wangefanya hivyo wangekufa (Mwanzo 2:17). Adamu alipaswa kumtii Mungu, na Mungu aliahidi uzima wa milele kwa utii wa Adamu. Hivyo katika kupokea Baraka ya uzima wa milele, kazi ya adamu ilikua ni kutii maagizo ya Mungu katika Agano hili.


Ni kwa masikitiko makubwa sana kuona kwamba pamoja na Adamu kupewa maelekezo yote haya, bado Adamu alivunja Agano hili na Mungu alipochukua tunda ambalo Hawa alimpa, na kulila, akikaidi amri ya Mungu na kuleta adhabu ya kifo kwa wanadamu wote ulimwenguni (Warumi 5:12-14). Na kifo hakikuwa kwa mwanadamu tu, bali hata kwa wanyama na mimea, na zaidi ya yote Adamu badala ya kutubu na kurejea kwa Mungu alielekeza lawama zote kwa mkewe, na mkewe naye akaelekeza lawama zote kwa yule nyoka (Mwanzo 3:12). Wakiufanya uumbaji wa Mungu kuwa ndio chanzo cha anguko lao.  Adamu na Hawa walikuwa wametangaza uhuru wao kwa tendo moja la uasi dhidi ya Mungu. Walichokifanya kilikuwa zaidi ya kula tu kipande cha tunda lililokatazwa. Kwa kiwango kikubwa, walikuwa wamekaidi amri iliyo wazi ya Mungu. Walichagua kusikiliza sauti ya kushawishi ya yule nyoka na kuruhusu kiburi chao wenyewe kuingia na kufanya kazi. Walifanya kosa kubwa la kupinga waziwazi haki ya Mungu katika kuyaongoza maisha yao, wakitumia mamlaka na uwezo juu ya maisha yao wenyewe.


Sehemu ya pili ya Agano hili tunaona jinsi Mungu anavyoshughulika na kuvunjwa kwa Agano lake na mwanadamu. Hata pamoja na mwanadamu kuanguka na Mungu kutoa adhabu ya kuwaondoa katika bustani ya Edeni, tunaona Mungu mwenye huruma na upendo kwa mwanadamu aliyemuumba kwa mfano wake mwenyewe akitoa ahadi nyingine ambayo itamrejesha mwanadamu katika uhusiano mzuri na Mungu. Kutokana na dhambi ya Adamu ya kutokutii, daima kutakuwepo na chuki kati ya Shetani na Hawa, na uzao wake. Mwanamke atazaa kwa uchungu, na kutakuwa na kutokuelewana vizuri kati ya mwanamume na mwanamke. Udongo utalaaniwa, miiba na michongoma itaonekana kwenye mimea, na kuishi kwa mwanadamu kutakuwa kwa taabu na dhiki kwa ulimwengu wote wa asili (Warumi 8:22-23), na mwishowe kifo kitakuwa hatima ya kila kiumbe hai (Mwanzo 3:14-19).


Licha ya hali ya kutisha ya laana hizi, na uharibifu uliotokea, ndani ya laana na uharibifu huu palikuweno ahadi. Akizungumza na Shetani, Mungu anasema “Nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino” (Mwanzo 3:15). Ni kweli kabisa kwamba mwanadamu humponda nyoka kichwa, na kugongwa na nyoka juu ya kisigino chake, lakini laana hii haikukusudiwa kwa nyoka tu. Ilinenwa kwa Shetani, kwa kutazamia ushindi wa Yesu Kristo katika kumkomboa mwanadamu na kuleta uzima wa milele. Uzao wa mwanamke ni Yesu Kristo, ambaye ingawa alichubuliwa na msalaba (Isaya 53:4-5), alimponda nyoka (Shetani) kichwa (Wagalatia 4:4, 1 Yohana 3:8).


Umuhimu wa Agano hili kwa Mkristo wa leo ni nini?


Ni vigumu sana kwa Mkristo kuelewa maana ya Agano jipya kama hana maarifa ya kutosha juu ya Agano hili ambalo Mungu alilifanya na Adamu bustanini Edeni, kwani kupitia Agano hili ndipo tunapoanza kuuona mpango wa Mungu katika kuleta ukombozi/wokovu kwa mwanadamu baada ya kuanguka katika dhambi. Hauwezi kuelewa sababu ya Kristo kufa msalabani endapo utakuwa umekosa maarifa juu ya Agano hili.


Katika Agano hili, Mungu anaahidi kumpa Adamu uzima wa milele ikiwa atamtii na kukataa kula tunda la mti uliokatazwa. Mungu alimwambia Adamu kwamba ikiwa yeye na mke wake wangetii amri hiyo wangeishi milele. Kupitia Agano hili tunaona kwamba baraka, uhisiano na Mungu, na uzima wa milele zilitegemea utii au “kazi” ya Adamu na Hawa bustanini Edeni.


Agano hili la matendo kati ya Mungu na Adamu bado lipo, lakini halina uwezo wa kuwaokoa wakosefu kwasababu halitoi msamaa wa dhambi wala uzima wa milele, katika Agano hili sisi ni wenye dhami na wafu. Tangu hapo awali baada ya kuanguka kwa mwanadamu katika dhambi hakuna mtu aliyeweza kushika masharti ya agano la kazi kwa sababu sisi sote, bila ubaguzi, tumezaliwa katika hatia ya dhambi ya kurithi ("dhambi ya asili"). Lakini kwao walioamini katika Kristo kuna habari njema, kwani agano la matendo limetimizwa! Yesu Kristo, Adamu wa Pili, alifanikiwa pale ambapo Adamu wa kwanza alishindwa.


Habari hizi tunazisoma katika kitabu cha Warumi 5:12–21, ambapo mistari hii inasema kwamba Yesu, Adamu wa mwisho, alitupatia uzima wa milele kwa utii Wake. Hivyo basi, ikiwa Adamu wa kwanza angalitii, yeye na wazao wake hawangekufa kamwe, bali wangeishi milele. Lakini kwa kushindwa kwake Adamu kutii, Kristo alitimiza agano hili kwa kutii kwake, na kupitia yeye mimi na wewe tuna uzima wa milele, na tupo katika uhusiano mzuri na Baba yetu wa Mbinguni. Na kama vile tulivyokufa katika dhambi ya Adamu, ndivyo tunavyoishi sasa kwa sababu ya utii wa Mwana wa Mungu.


Adamu alishindwa kutii katika Agano la Kale, Lakini Kristo alishinda katika Agano Jipya kwa kutii hadi kifo. Na kupitia yeye, kwa kutii kwake, mimi na wewe tuna uzima wa milele. Adamu alikuwa mtu wa kwanza, aliyeumbwa moja kwa moja na Mungu, kichwa cha mfano cha wanadamu. Yesu ndiye Mungu-mtu wa kwanza, Mwana wa moja kwa moja wa Mungu, Kichwa cha Kanisa. Adamu na Yesu waliingia ulimwenguni bila dhambi. Hata hivyo, ambapo Adamu alishindwa, Yesu alishinda.


Adamu alitenda dhambi mara moja, na hivyo kuwaangamiza wanadamu. Yesu alikufa mara moja, na hivyo kufunika wingi wa dhambi (Warumi 5:18-19).


Katika Agano la Mungu na Adamu tunajifunza kuwa, Mungu ni Mungu mwenye Upendo na Rehema. Kutoka kizazi hadi kizazi upendo na Rehema za Mungu kwetu zimeendelea kuonekana. Na tunajifunza pia kuwa, pamoja na madhaifu yetu yote Mungu ameendelea kututafuta na kujenga uhusiano wake nasi. Kila wakati Mungu ni Mwena, na Mungu ni mwema kila wakati.


Hatua gani tuchukue ili kuendelea kukaa hemani mwa Bwana?


Adamu alipewa machagu mawili ‘Uzima wa milele au Kifo’, kwa kukaidi kwake alichagua kifo na maisha yenye kujawa na taabu. Leo, baada ya muda mrefu, Mungu anataka tuchague, tuchague uzima wa milele katika Kristo. Ni kweli kwamba wanadamu wamepotoshwa na dhambi kiasi kwamba wanadamu hawamtafuti Mungu peke yao (Warumi 3:11-12), lakini tunajunza pia kuwa Mungu ameendelea kupinga matokeo haya ya dhambi kwa njia nyingi. (Matendo 10:34-35, Matendo 17:26-28, Warumi 2:14-15) na kwamba sura ya Mungu katika wanadamu haijapotea kabisa (Mwanzo 9:6). Kwa hiyo, kwa neema ya Mungu, bado tunaweza kuchagua. Sambamba na agano la Mungu na Adamu, injili ya Yesu Kristo inatuhimiza kufanya uchaguzi halisi leo.


Mungu aliwahimiza wana wa Israel “wachague uzima” (Kumbukumbu la Torati 30:19), Nasi tuchague uzima katika Kristo.


Kwasababu ya Kalvari mimi nimewekwa Huru,

Rumishael Ulomi

Copyright © www.kilicentric.com



Makala hii ipo kwa lugha ya KIINGEREZA HAPA

R

Rumishael Ulomi

Author, Coach & Minister

Rumishael Ulomi is a seasoned leader and minister dedicated to integrating Christian values into leadership and life. He empowers individuals to reach their God-given potential through discipleship, coaching, and mentorship.

KiliCentric

The official blogof Rumishael Ulomi aka RyChris, hailing all the way from Moshi Kilimanjaro. .

Search This Blog

Labels

Follow Us

Should Your Religion Be Based On Your Feelings? Here is the answer..

Should a person decide what to believe based on his or her feelings or something that does not change with moods and circumstances? Big question! Imagine Jesus of Nazareth nailed up on the cross, dying for our sins. Suppose He said, “This is not fun. I am not feeling anything good up here. Let me off this cross. I expected good feelings, not this! Pain is not where it is at for Me. My commitment to die to pay the penalty for man’s sin is far beyond what I am feeling right now.” How would you have counseled Jesus when the bad pain hit Him? Feelings based religion is shaky. Commitments based on good feelings are subject to change any day. This unbiblical approach would make all our commitments very tentative, unpredictable, shaky. This includes: marriage, family, job and friends. A marriage vow would only mean, “I’ll stay with you as long as my good feelings last. I expect only good times, no bad ones.” Jesus did not bail out when the going got tough. Some beliefs a Christian should also...

The second necessary step in designing a successful nonprofit strategy is knowing your beneficiaries

Last week I started a series of blog posts on building a strong and successful strategy for your nonprofit and I started with mentioning the first necessary step you will need to examine before kicking off with your strategy. If you haven’t read that post, I recommend that you visit the article HERE before continuing with this one. Having familiarity with the first article will help you understand this one even much better. This week we are looking at the second step to take when designing your nonprofit strategy, and that step in designing and building a strong and successful strategy for your nonprofit is clearly knowing, stating, and understanding who your beneficiaries are. Some organizations talk about beneficiaries, others refer to participants, others to clients, service users or partners. Here we will refer to beneficiaries as the people whom your nonprofit seeks to benefit. The reason why many nonprofit strategies fail is because too often nonprofits and funders ignore the con...

Being set free by the master who holds the keys to life

After Jesus died on the cross He went down to hell, crushed the devil, and took the keys of life. The devil held us prisoners to fear of death, but now we are given the chance to enjoy eternal life with God the father. The greatest gift the human race can ever earn. It’s all free of charge to be set free, for the master has promised to do this free of charge to all those who desire to be free. If you have not yet accepted Christ, then you are still in a prison cell and you need to be freed from this. The only way that can happen is if you humble yourself and come to the master who has the keys to set you free. If you are in the devils prison, you can’t save yourself, not matter how good you think you are in escaping. You will never be able to escape until you let the master who took the keys set you free. You will try million ways and times, but I assure you, you will never succeed on your own. Many of you may say ‘well I am free’, I can assure you that you are only free in the flesh; ...

Join the Sikio Sikivu Diary

Get weekly leadership insights, biblical management tools, and discipleship resources delivered straight to your inbox.

No spam, just wisdom. Unsubscribe anytime.